Return to search

Vitendawili vya Kiswahili: usambamba wake na dhima yake katika jamii

Vitendawili vya Kiswahili, kama vitendawili katika lugha nyingine za Kibantu, na kwa hakika katika lugha nyingine za Kiafrika, ni mafumbo ambayo hutolewa kama kauli au swali linalotaka jibu (Gowlett 1979; Harries 1971, 1976; Okpewho 1992). Vitendawili katika Kiswahili ni sehemu muhimu sana ya michezo ya watoto. Katika jamii ambazo bado zinaishi maisha ya jadi, watoto hukaa pamoja jioni pengine wakiwa na dada zao, kaka zao, na binamu zao wakasimuliana hadithi na kutegana vitendawili. Makala hii inachunguza muundo wa visabiki vya vitendawili vya Kiswahili na kutokana na mchangamano wa muundo tunapendekeza kwamba vitendawili ni njia kuu ya kufundisha watoto ufasaha wa lugha. Ukichunguza usambamba katika vitendawili utaona changamoto kubwa hutolewa kwa mtegaji na wasikilizaji wake kutokana na usambamba ulioko katika sintaksia, fonolojia, kadhalika sitiari. Kama Scheub (2002:124) asemavyo: «Vitendawili ni modeli kwa ajili sanaa za lugha».

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa:de:qucosa:11737
Date03 December 2012
CreatorsNgonyani, Deo
ContributorsMichigan State University, Universität Mainz
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageSwahili
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article, info:eu-repo/semantics/article, doc-type:Text
SourceSwahili Forum; 12(2005), S. 121-132
Rightsinfo:eu-repo/semantics/openAccess
Relationurn:nbn:de:bsz:15-qucosa-94062, qucosa:11593

Page generated in 0.0015 seconds