Return to search

Traditional Dances and Bongo Fleva: a Study of Youth Participation in Ngoma Groups in Tanzania

Kasi ya vijana katika kukuza muziki wa kizazi kipya katika kipindi cha utandawazi haiendani na kasi ya ukuzaji wa ngoma za asili. Mpaka sasa haujafanyika utafiti wa kina kuhusu kuzuka kwa tabia hii. Makala haya yanatumia mahojiano na vikundi vya ngoma vitatu halikadhalika wanamuziki wa kizazi kipya kuweka bayana chanzo cha tatizo. Aidha, makala haya yanatumia nadharia ya utendaji kama darubini kuchunguza matatizo ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni yanayowakumba vijana na namna yanavyochochea mfumuko wa tabia hii mpya. Utafiti huu umegundua kwamba uhaba wa mianya ya kiuchumi na kisiasa kwa vijana, nafasi ya ngoma za asili katika jamii ya sasa, mahusiano hasi kati ya vijana na wazee katika kuuendeleza utamaduni pamoja na vijana kutaka maendeleo ya haraka kuwa ndio chimbuko la tatizo.

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa:de:qucosa:12331
Date27 March 2014
CreatorsSanga, Daines
ContributorsUniversität Bayreuth, Universität Leipzig
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageEnglish
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article, info:eu-repo/semantics/article, doc-type:Text
SourceSwahili Forum 20 (2013), S. 67-84
Rightsinfo:eu-repo/semantics/openAccess
Relationurn:nbn:de:bsz:15-qucosa-138577, qucosa:12392

Page generated in 0.0023 seconds