Return to search

Mara tena juu ya usarufishaji (suala la mwana)

Dhana ya usarufishaji, kama Kamusi ya Isimu na Lugha inavyoeleza, ni ubadilishaji wa neno huru ama mofimu huru yenye maana ya kisemantiki na kuifanya mofimu funge na yenye maana ya kisarufi zaidi.
Tunaposema kuhusu usarufishaji, mara nyingi tunamaanisha hasa
ubadilishaji wa neno huru liwe mofimu. Miongoni mwa aina zote za maneno, ambazo zinaweza kusarufishwa, zile zinazotumika mara nyingi zaidi ni nomino na vitenzi. Ningetaka kujibu swali juu ya kazi ya kisarufi ya leksimu mwana: baada ya kuzichunguza maana zake za kisarufi inawezekana kutilia mkazo kwamba katika lugha ya Kiswahili tunashuhudia mwanzo wa kuibadilisha nomino huru mwana iwe kiambishi awali cha uundaji wa maneno mapya yanayotaja watu mbalimbali kutokana na kazi, shughuli zao, kuwepo katika vyama n.k. Inawezekana kwamba maneno ambatani yanayoanzia na mwana
yanaunda ngeli maalum ya nomino (sawa na ngeli ya 1a/2a ya lugha
nyingine za Kibantu).

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa.de:bsz:15-qucosa-98181
Date30 November 2012
CreatorsGromova, Nelli V.
ContributorsMoscow State Lomonosov University, Institute of Asian and African Studies, Universität zu Köln, Institut für Afrikanistik
PublisherUniversitätsbibliothek Leipzig
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageSwahili (individual language)
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article
Formatapplication/pdf
SourceSwahili Forum; 8(2001), S. 59-65

Page generated in 0.0033 seconds