Return to search

Habari za miti na mitishamba miongoni mwa Wamijikenda na Waswahili-matokeo ya kwanza kutoka utafiti

Utafiti ambao ni msingi wa habari hizo umefanywa katika miezi za Oktoba mpaka Disemba 2000 katika wilaya wa Kwale na Kilifi huko nchi ya Kenya. Wanachama wa timu ya utafiti wetu walikuwa Prof. F. Rottland, ambaye aliweka taratibu msamiati wa miti uliokusanywa, na Bw. Mohamed Pakia ambaye ni mwanabiolojia na aliyehojiana wanafunzi wa shule ya sekondari kuhusu ujuzi wa miti na mitishamba wao. Bw. Pakia ameshafanya kazi katika Coastal Forest Conservation Unit, yaani watu ambao husaidia wazee wa kimijikenda katika kuhifadhi misitu mitakatifu inayoitwa \"makaya\" na inatumiwa kwa matambiko na kama makaburi. Bw. Pakia ametambua: Ni hatari ya kupoteza ujuzi wa miti na mitishamba iliyotumiwa nanma ya kimila miongoni mwa wanafunzi wa shule ya sekondari: vijana hawajui matumizi ya mimea na pia wamepotea moyo wa kutaka kujua mambo hayo. Katika habari zifuatazo ninatoa mifano ya ule ujuzi wa watu wazima na wazee.

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa:de:qucosa:11727
Date30 November 2012
CreatorsSchulz-Burgdorf, Ulrich
ContributorsUniversität Bayreuth, Universität zu Köln
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageSwahili
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article, info:eu-repo/semantics/article, doc-type:Text
SourceSwahili Forum; 8(2001), S. 201-203
Rightsinfo:eu-repo/semantics/openAccess
Relationurn:nbn:de:bsz:15-qucosa-93705, qucosa:11588

Page generated in 0.0021 seconds