Return to search

Utegemezi au utegemeano baina ya Kenya na Tanzania katika ukuzaji na uendelezaji wa Kiswahili nchini Kenya?

Makala haya yanatathmini iwapo ukuzaji na uendelezaji wa Kiswahili nchini Kenya unategemea shughuli za kuiendeleza lugha hii zinazofanywa na Tanzania ama unatokana na kutegemeana baina ya mataifa haya katika kukikuza na kukiendeleza Kiswahili. Baadhi ya njia za kuiendeleza lugha zinajumuisha: kuisanifisha, kuifanyia utafiti na kuiimarisha kwa kuitungia kamusi, vitabu vya sarufi, kazi za kisanaa na kuitumia serikalini, mahakamani, katika elimu n.k. Makala haya yanaonyesha kuwa ingawa kuna utegemeano kati ya Kenya na Tanzania katika ukuzaji na uendelezaji wa Kiswahili, Tanzania inategemewa zaidi. Hususan inadhahirishwa kuwa Kenya imeitegemea Tanzania kwa kuagizia machapisho, wataalamu wa Kiswahili mbali na kutumia istilahi na hata kuchuma nafuu mifano ya Tanzania katika utumishi wa umma. Fauka ya hayo, inaonyeshwa kuwa pale ambapo Kenya haijafaidi kutokana na ufanisi wa Tanzania, ikiiga mfano wa Tanzania, upo uwezekano wa kufaulu.

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa:de:qucosa:11793
Date14 December 2012
CreatorsOyori Ogechi, Nathan
ContributorsMoi University, Universität zu Köln
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageSwahili
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article, info:eu-repo/semantics/article, doc-type:Text
SourceSwahili Forum; 9(2002), S. 155-172
Rightsinfo:eu-repo/semantics/openAccess
Relationurn:nbn:de:bsz:15-qucosa-93755, qucosa:11591

Page generated in 0.0018 seconds