Return to search

Mwingilianomatini katika tamthilia za Kiswahili: Mashetani na Kijiba cha Moyo

Tamthilia ya Kiswahili imedhihirisha, kwa njia moja au nyingine, uhusiano wa kimwingilianomatini. Makala haya yanadhamiria kuchunguza viwango na aina za mwingilianomatini baina ya tamthilia mbili za Kiswahili. Tamthilia hizi ni Mashetani (Hussein 1971) na Kijiba cha Moyo (Arege 2009). Tathmini hii inaongozwa na nadharia ya mwingilanomatini. Tumeteua na kuhakiki tamthilia hizi kwa misingi kwamba, kwa muda mrefu, Ebrahim Hussein ameaminika kuwa mmojawapo wa watunzi bora wa tamthilia ya Kiswahili katika eneo la Afrika Mashariki. Wahakiki wa fasihi wanaelekea kukubalia na kwamba Ebrahim Hussein ameathiri watunzi wengi wa baadaye wa tamthilia kimtindo, kimaudhui na usawiri wahusika. Lengo la makala haya ni kujaribu kuonesha jinsi tamthilia za Mashetani na Kijiba cha Moyo zinavyofanana kwa kuchunguza viwango vya mwingilianomatini baina ya tamthilia hizo kwa kurejelea, motifu, maudhui, matumizi ya lugha, na wahusika. Je, ni kwa kiwango gani mtunzi wa Kijiba cha Moyo ameathiriwa na mtunzi wa Mashetani? Je, amemnukuu, kudondoa au kumwiga mtangulizi wake kwa kiwango gani?

Identiferoai:union.ndltd.org:DRESDEN/oai:qucosa.de:bsz:15-qucosa-199683
Date30 March 2016
CreatorsNgesa, Ambrose K., Matundura, Enock, Kobia, John
ContributorsMoi University,, Universität Leipzig, Institut für Afrikanistik
PublisherUniversitätsbibliothek Leipzig
Source SetsHochschulschriftenserver (HSSS) der SLUB Dresden
LanguageSwahili (individual language)
Detected LanguageUnknown
Typedoc-type:article
Formatapplication/pdf
SourceSwahili Forum 22 (2015), S. 42-71

Page generated in 0.0024 seconds